Skip to main content

MAMA MJAMZITO ASILALIE TUMBO AU MGONGO

MAMA MJAMZITO ASILALIE TUMBO AU MGONGO

Kulalia mgongo sio vizuri kwa sababu uzito wa mtoto unazuia baadhi ya mishipa ya mgongoni inayosafirisha damu toka kwenye uti wa mgongo kwenda kichwani,na kutoka miguuni kuja kichwani kushindwa kusafirisha damu vizuri na kunabadili mfumo wa mzunguko wa damu  unaoweza kumuadhiri mama au mtoto.

ATHARI ZITOKANAZO NA MAMA MJAMZITO KULALIA MGONGO | CHALI | TUMBO.
∆ Kutokana na damu kushindwa kusafirishwa vizuri inapelekea kumsababishia mama mjamzito kupata matatizo kama,
∆ Kuvimba kwa misuli na inayo ambatana na maumivu (miguu na mikono)
∆ Kushuka au kupanda kwa blood pressure
∆ Ini kuelemewa uzito
∆ Kupunguza mzunguko wa damu ambayo ni hatari kwa uhai wa mtoto
∆ Kusikia kizunguzungu mara kwa mara
∆ Kama kupata kiungulio mara kwa mara nyakati za usiku
∆ Kukoroma
∆ Maumivu ya mgongo
∆ Mama na mtoto ushindwa kupumua vizuri kwa kusosa hewa (oxygen)
∆ Mtoto kukosa virutubisho vya kutosha.

MAMA ANASHAURIWA KULALIA MLALO GANI SALAMA
∆ Tafiti nyingi zinamshauri kwamba mama mjamzito alalie upande wa kushoto .Sababu damu husafirishwa kwa Urahisi zaidi kutoka kwenye moyo wa mama na kwenda kwenye kondo la mtoto na kumpa virutubisho vingi zaidi. .
∆ Iwapo mama atalalia tumbo au mgongo itamfanya mtoto asiwe comfortable atahangaika na kumpiga piga mama ili abadili position ya kulala.

USHAURI
∆ Mama anapolala ni vizuri akaweka mto katikati ya miguu usibane miguu ipitanishe, inakusaidia kulala comfortable,damu kusafirishwa vizuri na kutopata maumivu ya mgongo.Nyakati za usiku ni kawaida kwa watoto kupiga piga tumboni ,ila akipiga sana jua umelala vibaya anataka ubadilishe position.
                      
                        WELL - 0684127127 | 0743127127

Comments

Popular posts from this blog

ZIFAHAMU SABABU, DALILI, MATIBABU NA NAMNA YA KUZUIA TATIZO LA MIMBA ZABIBU | MOLAR PREGNANCY

ZIFAHAMU SABABU, DALILI, MATIBABU NA NAMNA YA KUZUIA TATIZO LA MIMBA ZABIBU | MOLAR PREGNANCY MIMBA ZABIBU: Ni uvimbe unaotokea baada ya mbegu ya kiume kurutubisha yai la kike kwenye mji wa mimba (uzazi). Uvimbe huu baada ya kutengenezwa huendelea kukua na kuongezeka ukubwa kama mimba ya kawaida. Baada ya muda flani huanza kuleta au kuonyesha dalili za mtu Mwenye mimba au mjamzito. Uvimbe huu umetengenezwa na Tishu au kuta za mji wa mimba au uzazi. Kwa kawaida hali hii au uvimbe huu unaweza ukawa saratani au usiwe saratani, awali huanza kawaida ila kwa baadae unaweza ukawa saratani (kansa). NAMNA INAVYOTOKEA | CHANZO | KISABABISHI. Kwa kawaida ili mimba itungwe lazima mbegu ya kiume ikutane na yai la kike, na pande zote mbili upande wa mbegu za kiume na wakike lazima kuwe na vinasaba. Kama yai la kike halina vinasaba hutengeneza mimba zabibu (molar pregnancy) inayojulikana kama partial molar pregnancy, uvimbe huu huendelea kuongezeka ukubwa kama fung...

Uhusiano kati ya kundi ya kundi la damu(blood group) na uchumba/Mimba/Ujauzito/ mtoto

Uhusiano kati ya kundi ya kundi la damu(blood group) na uchumba/Mimba/ Ujauzito / mtoto   1. Binadamu ana damu ambayo ina seli nyeupe, chembe sahani na sell nyekundu.. hizi seli nyekundu ndio zinabeba oksijeni na kabondayoksaidi na kimiminika chenyewe 2. Seli nyekundu zina protini inajishika ukutani mwake inaitwa antigen. kuna antigen A au B au seli inakuwa haina antigen      • Ambaye seli nyekundu zina antigen A, ana blood group A     • Ambaye seli nyekundu zina antigen B ana blood group B     • Ambaye seli zake zina Antigen A na B ana blood group AB      • Ambaye seli nyekundu hazina antigeni ana blood group O 3. katika seli hiyo hiyo nyekundu ikiwa na protini inayojishika katika ukuta wake, hii inaitwa D antigen maarufu kama Rh Factor  3.(a)     Mtu mwenye D antigen katika cell zake nyekundu, blood group yake inaandikwa na kuongezewa alama ya + mfano A+, B+, AB+ au O+ 3. ...

HATUA ZA UKUAJI WA MTOTO AKIWA TUMBONI

Je wewe ni mjamzito na unatamani kufahama Hatua ya ukuaji wa mtoto wako aliyeko tumboni ?? Hizi ndio Hatua za ukuaji wa mwanao akiwa tumboni. Hatua za ukuaji wa mtoto tumboni WIKI YA (1- 4). √  Yai la kike linarutubishwa na mbegu za kiume. √  Kijusi kinaanza kujitengeza (Umba) √  Mishipa ya damu,Tumbo,Ini, n.k vinatengenzwa WIKI YA (5 - 8). Viungo Muhimu vinatengenzwa na kukomaa √  Ubongo √  Moyo √  Uti wa Mgongo √  Macho,masikio,mdomo na pua. √  Miguu, mikono, vidole na kucha WIKI YA (9-12). √  Shingo huanza kujitengenza. √  Kope za macho hujitengeneza. √  Katika kipindi hiki mtoto anafikia urefu wa inchi 2.5 Kumb .... Uhitaji mwingi wa madini ya chuma kwa mtoto. WIKI YA (13-17). √  Miguu na mikono inakamilika √  Shingo inakamilika katika kipindi hiki. √  Mifupa inaanza kukomaa WIKI YA (18-22). √  Mtoto anaweza  Kusikia sauti za mama yake. √  Mtoto anaanza kucheza tumboni. ...