Skip to main content

ZIFAHAMU DALILI ZA HATARI KWA MAMA MJAMZITO

ZIFAHAMU DALILI ZA HATARI KWA MAMA MJAMZITO
Mama mjamzito yuko kwenye hatari ya kupata matatizo mengi yeye na mwanae.
Matatizo hayo kujitokeza kwa ishara au dalili tofauti tofauti kulingana na aina ya tatizo alilonalo Mama.
DALILI HIZI ZA HATARI KIPINDI CHA UJAUZITO NI.
• Kutokwa  na Damu ukeni
• Maumivu makali ya Tumbo
• Kuhisi kizungu zungu
• Maumivu makali ya kichwa
• Kutapika sana na kukosa hamu ya kula
• Kushindwa kuona
• Kupata degedege
• Kupata homa kali
• Mtoto kuacha kucheza | Kutokucheza siku nzima
• Chupa kupasuka bila uchungu kuanza
• Kutoa mkojo kidogo
Mama mjamzito aonapo Dalili hizi anatakiwa kutoa taarifa haraka na kwenda kituo cha Afya kilicho karibu yake kwa.
• Uchunguzi wa kina
• Matibabu ya haraka
VIPIMO VYA MUHIMU KIPIMA KIPINDI CHA UJAUZITO NI.
• Kipimo cha Kaswende
• Kipimo cha damu kuangalia wingi wa damu
• Kipimo cha mkojo kuangalia wingi wa protini na maambukizi ya njia ya mkojo.
• Kipimo cha damu kuangalia group lako la damu Na mmeo
• Kipimo cha malaria
• Kipimo cha UKIMWI Kuangalia kama una maambukizi ili umkinge mtoto asipate maambukizi Wakati wa ujauzito, kujifungua na Wakati wa kunyonyesha.
• Kipimo cha haja kubwa kuangalia maambukizi ya minyoo
Mama ubainikapo unatatizo lolote hapo juu Jitahidi kuanza dawa ili kuepuka madhara na Magonjwa yapatikanayo kupitia Maradhi hayo.
Usiache kucomment hapo chini kwa maswali na ushauri.
Wasiliana nasi kwa Ushauri na Matibabu kwa Namba 0684/0743127127

Comments

  1. Mim ni mjamzito mimbq yangu inawiki 7 ila tangu jumanne naona damu kidogo nikienda choosing nikaenda hospital nikawaeleze wakanipima pia nikapiga ultrasound ikaonekana ipo vizuri na sasa bado naona damu kidogo nikienda chooni naombeni msaada weni

    ReplyDelete
  2. Mim mbna nahis kunavuta chini ya kitovu

    ReplyDelete
  3. This comment has been removed by the author.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

IFAHAMU ARGI PLUS (+) MAANA YAKE | KAZI ZAKE | FAIDA ZAKE | MATUMIZI YAKE

IFAHAMU ARGI PLUS (+) MAANA YAKE | KAZI ZAKE | FAIDA ZAKE | MATUMIZI YAKE FOREVER Argi+ ni bidhaa bora kabisa kutoka katika kampuni yetu ya Forever living products Ina L-arginine amino acid kwa kila kijiko kimoja cha Argi+ Ina Nitric oxide ambayo inasaidia kutanua mishipa ya damu hivyo kuruhusu damu kupita vizuri Ina viondosha sumu vya *POMOGRANATE* ambavyo ni muhimu sana ili kuondoa sumu mwilini Ina *Vitamin* *Complex* ambazo zinasaidia kujenga misuli FAIDA ZA KUTUMIA ARGI+ 1. Ni kirutubisho muhimu sana kutumiwa kila siku kwa ajiili ya kusaidia mifumo yote ya mwili ili kuupa mwili uwezo wa kufanya kazi vizui zaidi. 2. Inasaidia mfumo wa kinga ya mwili, kutokana na nitric oxide ambayo inatumiwa na chembechembe nyeupe za damu kuua bacteria. Hivyo kuupa mwili uwezo zaidi wa kupigana na magonjwa. 3. Inasaidia kurekebisha kiwango cha "blood pressure kiwe sahihi na afya ya mzunguko wa damu ya moyo kiujumla. 4. Inasaidia kutengenezwa kwa mifupa na mwili kiujumla hivyo ...

ZIFAHAMU SABABU, DALILI, MATIBABU NA NAMNA YA KUZUIA TATIZO LA MIMBA ZABIBU | MOLAR PREGNANCY

ZIFAHAMU SABABU, DALILI, MATIBABU NA NAMNA YA KUZUIA TATIZO LA MIMBA ZABIBU | MOLAR PREGNANCY MIMBA ZABIBU: Ni uvimbe unaotokea baada ya mbegu ya kiume kurutubisha yai la kike kwenye mji wa mimba (uzazi). Uvimbe huu baada ya kutengenezwa huendelea kukua na kuongezeka ukubwa kama mimba ya kawaida. Baada ya muda flani huanza kuleta au kuonyesha dalili za mtu Mwenye mimba au mjamzito. Uvimbe huu umetengenezwa na Tishu au kuta za mji wa mimba au uzazi. Kwa kawaida hali hii au uvimbe huu unaweza ukawa saratani au usiwe saratani, awali huanza kawaida ila kwa baadae unaweza ukawa saratani (kansa). NAMNA INAVYOTOKEA | CHANZO | KISABABISHI. Kwa kawaida ili mimba itungwe lazima mbegu ya kiume ikutane na yai la kike, na pande zote mbili upande wa mbegu za kiume na wakike lazima kuwe na vinasaba. Kama yai la kike halina vinasaba hutengeneza mimba zabibu (molar pregnancy) inayojulikana kama partial molar pregnancy, uvimbe huu huendelea kuongezeka ukubwa kama fung...