LISHE WAKATI WA UJAUZITO NA WAKATI WA KUNYONYESHA.
Kipindi chote cha Ujauzito na wakati wa kunyonyesha Mama anahitajika kupata chakula cha kutosha kwa ajili ya Kiumbe kilicho tumboni pamoja na mama mwenyewe.
Mama anaye nyonyesha anahitaji mlo ulio sahihi kwa ajili ya kusaidia kupata maziwa ya kutosha kwa ajili ya mtoto na kukupa nguvu na virutubisho vyote muhimu mwilini.
FAIDA ZA LISHE BORA
• Husaidia kuongeza damu na kuzuia upungufu wa damu
• Husaidia kuongeza uzito kulingana na umri wa mama na mtoto na kuzuia kupata Utapiamlo.
• Huimalisha ukuaji wa mtoto kimwili na kiakili.
• Husaidia kuzuia kupata mtoto mwenye uzito pungufu.
• Humsaidia mama kuandaa mwili na utengenezaji wa maziwa ya kutosha wakati wa kunyonyesha.
MAMBO YA KUZINGATIA.
• Kabla ya kuweka chochote kinywani na baada ya kutumia choo nawa mikono yako kwa maji safi na Salama na sabuni.
• Anza kuhudhuria kliniki mapema baada ya kuhisi ni mjamzito na mpeleke mtoto kliniki mapema kwa ajili ya chanjo.
• Pata muda wa kutosha wa kupumzika • Tumia chandarua chenye dawa.
• Tumia dawa za minyoo , Malaria, na kuongeza damu.
• Epuka kutumia pombe na sigara, Tumbaku.
• Tumia sana mboga mboga na matunda pia, Osha vizuri Matunda na mboga mboga za majani kabla ya kizipika
• Hakikisha vyombo vya chakula ni visafi na vikavu.
NAMNA YA KUPANGILIA NA KUANDAA CHAKULA /MLO WAKO KILA SIKU.
Itaendelea.............
Karibu kwa maswali, Maoni
Wasiliana nasi kwa namba 0684127127 | 0743127127
Comments
Post a Comment