Skip to main content

KUZIBA KWA MIRIJA YA UZAZI KWA MWANAMKE

KUZIBA KWA MIRIJA YA UZAZI

KUZIBA KWA MIRIJA YA UZAZI Ni moja ya sababu inayopelekea mwanamke Kushindwa kubeba /kushika mimba.

- Mirija ya Uzazi ina weza kuziba kwa sababu mbali mbali.
- Kuziba kwa mirija ya uzazi ni moja ya sababu kubwa ya Ugumba kwa wanawake.

SABABU ZINAZOWEZA PELEKEA MWANAMKE KUZIBA KWA MIRIJA YA UZAZI NI...

- Kuwa na Uvimbe ambao umeota kwenye mirija ya uzaziz
- Kuwa na Ugonjwa wa maambukizi ya kizazi na Nyonga.
- Kuwa na historia ya mimba kutunga nje ya kizazi.
- Magonjwa ya zinaa na upasuaji wa tumbo au uvimbe kwenye ukuta wa uzazi.
- Kuwa na maambukizi kwenye mirija yaliyo sababishwa na utoaji wa mimba, kupasuka kwa kidole tumbo.
- Uzazi wa mpango (Lupu/Kitanzi)
- Ajari iliyo husisha Tumbo.
- Mirija kujaa maji.

DALILI ZA KUZIBA KWA MIRIJA YA UZAZI

- Maumivu wakati wa kujamiana /Tendo
- Maumivu makali ya nyonga na Tumbo kwa chini.
- Kupata hedhi matone ikiambatana na Maumivu makali/Kupata damu nyingi Wakati wa hedhi.
- Maumivu makali wakati wa kukojoa
- Maumivu makali ya Mugongo kwa chini/Kiuno
- Kuchoka sana

VIPIMO | MATIBABU | NAMNA YA KUZUIA /KUJIKINGA

- Vipimo vinapatikana kwenye vituo vya Afya Baada ya uchunguzi na Maelezo.
- Kipimo cha picha ya Tumbo
- Kipimo cha damu.
- Kipimo cha mkojo
- Matibabu hutolewa na mtoa Huduma wa Afya baada ya Maelezo na uchunguzi wa kina

NAMNA YA KUZUIA/KUJIKINGA
- Epuka utoaji mimba
- Tibu mapema magonjwa ya zinaa
- Chunguza/Pima Afya Mara kwa Mara.
- Wahi kituo cha Afya uonapo dalili kama hizi.
- Tumia Dozi kikamilifu

Kwa Maelezo na ushauri,Maswali andika hapa chini..

Kwa Maelezo zaidi wasiliana nasi kwa namba 0684127127-0743127127
WhatsApp :

Comments

Popular posts from this blog

IFAHAMU ARGI PLUS (+) MAANA YAKE | KAZI ZAKE | FAIDA ZAKE | MATUMIZI YAKE

IFAHAMU ARGI PLUS (+) MAANA YAKE | KAZI ZAKE | FAIDA ZAKE | MATUMIZI YAKE FOREVER Argi+ ni bidhaa bora kabisa kutoka katika kampuni yetu ya Forever living products Ina L-arginine amino acid kwa kila kijiko kimoja cha Argi+ Ina Nitric oxide ambayo inasaidia kutanua mishipa ya damu hivyo kuruhusu damu kupita vizuri Ina viondosha sumu vya *POMOGRANATE* ambavyo ni muhimu sana ili kuondoa sumu mwilini Ina *Vitamin* *Complex* ambazo zinasaidia kujenga misuli FAIDA ZA KUTUMIA ARGI+ 1. Ni kirutubisho muhimu sana kutumiwa kila siku kwa ajiili ya kusaidia mifumo yote ya mwili ili kuupa mwili uwezo wa kufanya kazi vizui zaidi. 2. Inasaidia mfumo wa kinga ya mwili, kutokana na nitric oxide ambayo inatumiwa na chembechembe nyeupe za damu kuua bacteria. Hivyo kuupa mwili uwezo zaidi wa kupigana na magonjwa. 3. Inasaidia kurekebisha kiwango cha "blood pressure kiwe sahihi na afya ya mzunguko wa damu ya moyo kiujumla. 4. Inasaidia kutengenezwa kwa mifupa na mwili kiujumla hivyo ...

ZIFAHAMU SABABU, DALILI, MATIBABU NA NAMNA YA KUZUIA TATIZO LA MIMBA ZABIBU | MOLAR PREGNANCY

ZIFAHAMU SABABU, DALILI, MATIBABU NA NAMNA YA KUZUIA TATIZO LA MIMBA ZABIBU | MOLAR PREGNANCY MIMBA ZABIBU: Ni uvimbe unaotokea baada ya mbegu ya kiume kurutubisha yai la kike kwenye mji wa mimba (uzazi). Uvimbe huu baada ya kutengenezwa huendelea kukua na kuongezeka ukubwa kama mimba ya kawaida. Baada ya muda flani huanza kuleta au kuonyesha dalili za mtu Mwenye mimba au mjamzito. Uvimbe huu umetengenezwa na Tishu au kuta za mji wa mimba au uzazi. Kwa kawaida hali hii au uvimbe huu unaweza ukawa saratani au usiwe saratani, awali huanza kawaida ila kwa baadae unaweza ukawa saratani (kansa). NAMNA INAVYOTOKEA | CHANZO | KISABABISHI. Kwa kawaida ili mimba itungwe lazima mbegu ya kiume ikutane na yai la kike, na pande zote mbili upande wa mbegu za kiume na wakike lazima kuwe na vinasaba. Kama yai la kike halina vinasaba hutengeneza mimba zabibu (molar pregnancy) inayojulikana kama partial molar pregnancy, uvimbe huu huendelea kuongezeka ukubwa kama fung...

ZIFAHAMU DALILI ZA HATARI KWA MAMA MJAMZITO

ZIFAHAMU DALILI ZA HATARI KWA MAMA MJAMZITO Mama mjamzito yuko kwenye hatari ya kupata matatizo mengi yeye na mwanae. Matatizo hayo kujitokeza kwa ishara au dalili tofauti tofauti kulingana na aina ya tatizo alilonalo Mama. DALILI HIZI ZA HATARI KIPINDI CHA UJAUZITO NI . • Kutokwa  na Damu ukeni • Maumivu makali ya Tumbo • Kuhisi kizungu zungu • Maumivu makali ya kichwa • Kutapika sana na kukosa hamu ya kula • Kushindwa kuona • Kupata degedege • Kupata homa kali • Mtoto kuacha kucheza | Kutokucheza siku nzima • Chupa kupasuka bila uchungu kuanza • Kutoa mkojo kidogo Mama mjamzito aonapo Dalili hizi anatakiwa kutoa taarifa haraka na kwenda kituo cha Afya kilicho karibu yake kwa. • Uchunguzi wa kina • Matibabu ya haraka VIPIMO VYA MUHIMU KIPIMA KIPINDI CHA UJAUZITO NI . • Kipimo cha Kaswende • Kipimo cha damu kuangalia wingi wa damu • Kipimo cha mkojo kuangalia wingi wa protini na maambukizi ya njia ya mkojo. • Kipimo cha damu kuangalia gr...