Skip to main content

MADHARA YA KUSHIRIKI TENDO LA NDOA WAKATI WA HEDHI.

Kufanya mapenzi/kushiriki tendo wakati wa hedhi ni kitendo cha kujiusisha na mapenzi na msichana au mwanamke aliye katika siku zake za kisichana.

Kuna madhara mengi yanaweza yakatokea na kwa kawaida si mazuri kwa afya ya wote wawili.Hivyo kwa ushauri huwa tunapenda watu wajari sana afya zao na si kuzidumaza na kuendekeza hisia kwani hiloo ndilo kosa kubwa la vijana wengi wa siku hizi.

Yafatayo ni baadhi ya madhara yanayoweza kutokea endapo wawili hawa wakafanya ngono wakati mwanamke yupo katika siku zake {period}

 MADHARA KWA MWANAUME.

1. Kupata maambukizi katika njia ya mkojo hadi kwenye kibofu.  

2. Maambukizi katika tezi dume(Prostetits) hii inaweza kuathiri mfumo wa uzazi wa mwanaume.  

3. Kuziba kwa njia ya mkojo.  

4. Utasa au ugumba.  

5. Ulegevu wa misuli ya uume na upungufu wa nguvu za kiume.  

6. Athari mbaya ya kisaikolojia kwa kuwa anafanya tendo katika mazingira machafu hali itakayompelekea kutolifurahia tendo kutokana na hali ya umaji maji,utelezi, au harufu kali na mbaya na hivyo kuona kuwa mwanamke ni mchafu.Pia hali hii ikizidi inaweza kuathiri hata hufanyaji wa tendo katika siku za kawaida zisizo za hedhi.

MADHARA KWA MWANAMKE.

1. Kupatwa na mambukizi viungo vya ndanivya uzazi  kama vile  shingo ya kizazi,mirija ya uzazi kwa ujumla wake anaweza kuwa na tatizo la PID( PELVIC INFLAMATORY DISEASES) tatizo ambalo linaweza kuathiri mfumo wake wa uzazi.  

2. Maumivu makali ya tumbo hasa kwa wale wanaopatwa na maumivu wakati wa hedhi.(Dysmenorrhea).

3. Utokaji wa damu unaweza ukaongeza kuliko vile inavyotoka kwa kawaida yake.  

4. Utasa au Ugumba.  

5. Kuvimba kwa kuta za ndani za uke kwa kuwa wakati wa hedhi zenyewe huwa tayari zimevimba au kutanunuka hali pia itamsababishia maumivu kwenye uke wakati wa tendo la ndoa.  

6. Athari mbaya ya kisaikolojia:
Mwanamke atahisi kuwa mumewe hamjali wala mpendi bali anajali hisia zake za kingono na kwamba yeye anatumika kingono tu.
Pia kuona kuwa mumewe ajali afya yake pamoja na maumivu anayoyapata lakini bado huyu mume anataka hushiriki

Kwa mawasiliano zaidi 0684127127 | 0743127127

Kwa maoni na ushauri/maswali usisahau kutuandikia hapa chini.

Comments

Popular posts from this blog

ZIFAHAMU SABABU, DALILI, MATIBABU NA NAMNA YA KUZUIA TATIZO LA MIMBA ZABIBU | MOLAR PREGNANCY

ZIFAHAMU SABABU, DALILI, MATIBABU NA NAMNA YA KUZUIA TATIZO LA MIMBA ZABIBU | MOLAR PREGNANCY MIMBA ZABIBU: Ni uvimbe unaotokea baada ya mbegu ya kiume kurutubisha yai la kike kwenye mji wa mimba (uzazi). Uvimbe huu baada ya kutengenezwa huendelea kukua na kuongezeka ukubwa kama mimba ya kawaida. Baada ya muda flani huanza kuleta au kuonyesha dalili za mtu Mwenye mimba au mjamzito. Uvimbe huu umetengenezwa na Tishu au kuta za mji wa mimba au uzazi. Kwa kawaida hali hii au uvimbe huu unaweza ukawa saratani au usiwe saratani, awali huanza kawaida ila kwa baadae unaweza ukawa saratani (kansa). NAMNA INAVYOTOKEA | CHANZO | KISABABISHI. Kwa kawaida ili mimba itungwe lazima mbegu ya kiume ikutane na yai la kike, na pande zote mbili upande wa mbegu za kiume na wakike lazima kuwe na vinasaba. Kama yai la kike halina vinasaba hutengeneza mimba zabibu (molar pregnancy) inayojulikana kama partial molar pregnancy, uvimbe huu huendelea kuongezeka ukubwa kama fung...

Uhusiano kati ya kundi ya kundi la damu(blood group) na uchumba/Mimba/Ujauzito/ mtoto

Uhusiano kati ya kundi ya kundi la damu(blood group) na uchumba/Mimba/ Ujauzito / mtoto   1. Binadamu ana damu ambayo ina seli nyeupe, chembe sahani na sell nyekundu.. hizi seli nyekundu ndio zinabeba oksijeni na kabondayoksaidi na kimiminika chenyewe 2. Seli nyekundu zina protini inajishika ukutani mwake inaitwa antigen. kuna antigen A au B au seli inakuwa haina antigen      • Ambaye seli nyekundu zina antigen A, ana blood group A     • Ambaye seli nyekundu zina antigen B ana blood group B     • Ambaye seli zake zina Antigen A na B ana blood group AB      • Ambaye seli nyekundu hazina antigeni ana blood group O 3. katika seli hiyo hiyo nyekundu ikiwa na protini inayojishika katika ukuta wake, hii inaitwa D antigen maarufu kama Rh Factor  3.(a)     Mtu mwenye D antigen katika cell zake nyekundu, blood group yake inaandikwa na kuongezewa alama ya + mfano A+, B+, AB+ au O+ 3. ...

ALL BEAUTIFUL SCRUBS (SURGICAL GOWNS)  AND MEDICAL | LAB- COATS FOR MALE  AND FEMALE ARE AVAILABLE

GOOD NEWS TO YOU : ALL BEAUT IFUL SCRUBS (SURGICAL GOWNS)  AND LAB COATS FOR MALE  AND FEMALE ARE AVAILABLE TO US ,SO ITS YOUR TIME NOW TO CONTACT US FOR GOOD SERVICES 0THER EQUIPMENTS ARE LIKE STETHOSCOPE ♦ Littman class II ♦ Littman master class II ♦ Littman class III ♦ Dual head stethoscope ♦ Transparent Sprague Rappaport stethoscope ♦ MDF Stethoscope (Adult) ♦ MDF deluxe Infant and Neonate Stethoscope ♦ Stainless Steel stethoscope For Adult TAPE MEASURES of different in morden  types BP MACHINE ♦ Upper  arm automatic digital blood pressure monitor ♦ Wrist type automatic digital pressure monitor ♦ Upper arm automatic digital blood pressure monitor ♦ Aneroid sphygmomanometer -Palm Type Sphygmomanometer ♦ Palm Type Sphygmomanometer -Bokang Sphygmomanometer ♦ Splenger Blood pressure monitor -Riesta Blood pressure Monitor -Omrin Semi automatic blood pressure monitor REFLEX HUMMER ( PATELLA HUMMER) ♦ General reflex hummer  ♦ Fallow hummer...