Skip to main content

MAAMBUKIZI YA FANGASI KIPINDI CHA UJAUZITO | KIFAHAMU CHANZO | CHANZO | DALILI | UCHUNGUZI | MATIBABU | NAMNA YA KUJIKINGA.

MAAMBUKIZI YA FANGASI KIPINDI CHA UJAUZITO | KIFAHAMU CHANZO | CHANZO  | DALILI   | UCHUNGUZI  | MATIBABU | NAMNA YA KUJIKINGA.

FANGASI Ni maambukizi yanayoweza Jittokeza sehemu yoyote ya mwili.
Kuna aina kadha wa kadha ya fangasi na majina hutegemea na sehemu ya mwili walipo.

FANGASI WA UKENI - KIPINDI CHA UJAUZITO
Hawa ni moja ya fangasi ambao husumbua na hujitokeza kwa Wajawazito au kipindi cha Ujauzito na hushambulia sehemu ya uke.

Fangasi ambao hushambulia kipindi cha ujauzito wanajulikana kwa jina la candida albicans
Kipindi cha Ujauzito kuna mabdiliko ya Homoni ambazo kupelekea kubadilika kwa uasidi na ualikali (PH) ya Uke, na kuruhusu fangasi kuota kirahisi.

Kipindi cha ujauzito homoni aina ya estrojeni(estrogen) inakuwa nyingi kuliko zingine na kufanya mazingira rafiki kwa fangasi kuota.

Kuna sababu kadha wa kadha ambazo zinapelekea mjamzito kupata fangasi Mara kwa Mara .

CHANZO | SABABU
• Matumizi ya Dawa aina ya antibiotics Mara kwa Mara na kwa muda mrefu.
• Kuosha uke kwa maji na sabuni Mara kwa Mara (douching)
• Mabadiliko ya homoni kipindi cha ujauzito
• Matumizi ya vitu kama pafyumu au malashi, losheni kwenye uke.

DALILI
• Kuwasha ukeni
• Kutokwa na uchafu mweupe mzito kama maziwa mgando usio na harufu.
• Kuhisi Maumivu wakati wa kujamiana
• Kusikia maumivu kama vidonda wakati wa kujisaidia haja kubwa.

MADHARA YA FANGASI KWA MTOTO
• Mtoto kudumaa tumboni
• Mtoto kufia tumboni
• Matatizo ya kupumua
• Mtoto njiti
• Mtoto kuzaliwa na kilo ndogo
• Mtoto Wakati wa kuzaliwa anaweza kupata maambukizi ya fangasi na kuadhili Afya yake na ukuaji wake.

UCHUNGUZI NA MATIBABU NA NAMNA YA KUJIKINGA
• Mjamzito mewnye dalili kama hizi anashauriwa kufanyiwa vipimo vya maabara
• Mjamzito baada ya kuchunguzwa na kubainika anatatizo hilo anapewa dawa za kupachika ukeni.
• Epuka kuosha uke kwa maji na sabuni Mara kwa Mara.
• Safisha uke kwa kitambaa safi na kikavu.
• Tibu tatizo mapema kabla halijawa kubwa.
• Epuka Matumizi ya pafyumu, lotioni ukeni.
• Epuka Matumizi ya dawa bila ushauri wa daktari.
• Tumia nguo za ndani aina ya pamba
•  Jisafishe kutoka mbele kwenda nyuma baada ya kujisaidia haja kubwa.
• Epuka nguo za kubana.

Comments

Popular posts from this blog

IFAHAMU ARGI PLUS (+) MAANA YAKE | KAZI ZAKE | FAIDA ZAKE | MATUMIZI YAKE

IFAHAMU ARGI PLUS (+) MAANA YAKE | KAZI ZAKE | FAIDA ZAKE | MATUMIZI YAKE FOREVER Argi+ ni bidhaa bora kabisa kutoka katika kampuni yetu ya Forever living products Ina L-arginine amino acid kwa kila kijiko kimoja cha Argi+ Ina Nitric oxide ambayo inasaidia kutanua mishipa ya damu hivyo kuruhusu damu kupita vizuri Ina viondosha sumu vya *POMOGRANATE* ambavyo ni muhimu sana ili kuondoa sumu mwilini Ina *Vitamin* *Complex* ambazo zinasaidia kujenga misuli FAIDA ZA KUTUMIA ARGI+ 1. Ni kirutubisho muhimu sana kutumiwa kila siku kwa ajiili ya kusaidia mifumo yote ya mwili ili kuupa mwili uwezo wa kufanya kazi vizui zaidi. 2. Inasaidia mfumo wa kinga ya mwili, kutokana na nitric oxide ambayo inatumiwa na chembechembe nyeupe za damu kuua bacteria. Hivyo kuupa mwili uwezo zaidi wa kupigana na magonjwa. 3. Inasaidia kurekebisha kiwango cha "blood pressure kiwe sahihi na afya ya mzunguko wa damu ya moyo kiujumla. 4. Inasaidia kutengenezwa kwa mifupa na mwili kiujumla hivyo ...

ZIFAHAMU SABABU, DALILI, MATIBABU NA NAMNA YA KUZUIA TATIZO LA MIMBA ZABIBU | MOLAR PREGNANCY

ZIFAHAMU SABABU, DALILI, MATIBABU NA NAMNA YA KUZUIA TATIZO LA MIMBA ZABIBU | MOLAR PREGNANCY MIMBA ZABIBU: Ni uvimbe unaotokea baada ya mbegu ya kiume kurutubisha yai la kike kwenye mji wa mimba (uzazi). Uvimbe huu baada ya kutengenezwa huendelea kukua na kuongezeka ukubwa kama mimba ya kawaida. Baada ya muda flani huanza kuleta au kuonyesha dalili za mtu Mwenye mimba au mjamzito. Uvimbe huu umetengenezwa na Tishu au kuta za mji wa mimba au uzazi. Kwa kawaida hali hii au uvimbe huu unaweza ukawa saratani au usiwe saratani, awali huanza kawaida ila kwa baadae unaweza ukawa saratani (kansa). NAMNA INAVYOTOKEA | CHANZO | KISABABISHI. Kwa kawaida ili mimba itungwe lazima mbegu ya kiume ikutane na yai la kike, na pande zote mbili upande wa mbegu za kiume na wakike lazima kuwe na vinasaba. Kama yai la kike halina vinasaba hutengeneza mimba zabibu (molar pregnancy) inayojulikana kama partial molar pregnancy, uvimbe huu huendelea kuongezeka ukubwa kama fung...

ZIFAHAMU DALILI ZA HATARI KWA MAMA MJAMZITO

ZIFAHAMU DALILI ZA HATARI KWA MAMA MJAMZITO Mama mjamzito yuko kwenye hatari ya kupata matatizo mengi yeye na mwanae. Matatizo hayo kujitokeza kwa ishara au dalili tofauti tofauti kulingana na aina ya tatizo alilonalo Mama. DALILI HIZI ZA HATARI KIPINDI CHA UJAUZITO NI . • Kutokwa  na Damu ukeni • Maumivu makali ya Tumbo • Kuhisi kizungu zungu • Maumivu makali ya kichwa • Kutapika sana na kukosa hamu ya kula • Kushindwa kuona • Kupata degedege • Kupata homa kali • Mtoto kuacha kucheza | Kutokucheza siku nzima • Chupa kupasuka bila uchungu kuanza • Kutoa mkojo kidogo Mama mjamzito aonapo Dalili hizi anatakiwa kutoa taarifa haraka na kwenda kituo cha Afya kilicho karibu yake kwa. • Uchunguzi wa kina • Matibabu ya haraka VIPIMO VYA MUHIMU KIPIMA KIPINDI CHA UJAUZITO NI . • Kipimo cha Kaswende • Kipimo cha damu kuangalia wingi wa damu • Kipimo cha mkojo kuangalia wingi wa protini na maambukizi ya njia ya mkojo. • Kipimo cha damu kuangalia gr...