Skip to main content

MAAMBUKIZI YA FANGASI KIPINDI CHA UJAUZITO | KIFAHAMU CHANZO | CHANZO | DALILI | UCHUNGUZI | MATIBABU | NAMNA YA KUJIKINGA.

MAAMBUKIZI YA FANGASI KIPINDI CHA UJAUZITO | KIFAHAMU CHANZO | CHANZO  | DALILI   | UCHUNGUZI  | MATIBABU | NAMNA YA KUJIKINGA.

FANGASI Ni maambukizi yanayoweza Jittokeza sehemu yoyote ya mwili.
Kuna aina kadha wa kadha ya fangasi na majina hutegemea na sehemu ya mwili walipo.

FANGASI WA UKENI - KIPINDI CHA UJAUZITO
Hawa ni moja ya fangasi ambao husumbua na hujitokeza kwa Wajawazito au kipindi cha Ujauzito na hushambulia sehemu ya uke.

Fangasi ambao hushambulia kipindi cha ujauzito wanajulikana kwa jina la candida albicans
Kipindi cha Ujauzito kuna mabdiliko ya Homoni ambazo kupelekea kubadilika kwa uasidi na ualikali (PH) ya Uke, na kuruhusu fangasi kuota kirahisi.

Kipindi cha ujauzito homoni aina ya estrojeni(estrogen) inakuwa nyingi kuliko zingine na kufanya mazingira rafiki kwa fangasi kuota.

Kuna sababu kadha wa kadha ambazo zinapelekea mjamzito kupata fangasi Mara kwa Mara .

CHANZO | SABABU
• Matumizi ya Dawa aina ya antibiotics Mara kwa Mara na kwa muda mrefu.
• Kuosha uke kwa maji na sabuni Mara kwa Mara (douching)
• Mabadiliko ya homoni kipindi cha ujauzito
• Matumizi ya vitu kama pafyumu au malashi, losheni kwenye uke.

DALILI
• Kuwasha ukeni
• Kutokwa na uchafu mweupe mzito kama maziwa mgando usio na harufu.
• Kuhisi Maumivu wakati wa kujamiana
• Kusikia maumivu kama vidonda wakati wa kujisaidia haja kubwa.

MADHARA YA FANGASI KWA MTOTO
• Mtoto kudumaa tumboni
• Mtoto kufia tumboni
• Matatizo ya kupumua
• Mtoto njiti
• Mtoto kuzaliwa na kilo ndogo
• Mtoto Wakati wa kuzaliwa anaweza kupata maambukizi ya fangasi na kuadhili Afya yake na ukuaji wake.

UCHUNGUZI NA MATIBABU NA NAMNA YA KUJIKINGA
• Mjamzito mewnye dalili kama hizi anashauriwa kufanyiwa vipimo vya maabara
• Mjamzito baada ya kuchunguzwa na kubainika anatatizo hilo anapewa dawa za kupachika ukeni.
• Epuka kuosha uke kwa maji na sabuni Mara kwa Mara.
• Safisha uke kwa kitambaa safi na kikavu.
• Tibu tatizo mapema kabla halijawa kubwa.
• Epuka Matumizi ya pafyumu, lotioni ukeni.
• Epuka Matumizi ya dawa bila ushauri wa daktari.
• Tumia nguo za ndani aina ya pamba
•  Jisafishe kutoka mbele kwenda nyuma baada ya kujisaidia haja kubwa.
• Epuka nguo za kubana.

Comments

Popular posts from this blog

MAMA MJAMZITO ASILALIE TUMBO AU MGONGO

MAMA MJAMZITO ASILALIE TUMBO AU MGONGO Kulalia mgongo sio vizuri kwa sababu uzito wa mtoto unazuia baadhi ya mishipa ya mgongoni inayosafirisha damu toka kwenye uti wa mgongo kwenda kichwani,na kutoka miguuni kuja kichwani kushindwa kusafirisha damu vizuri na kunabadili mfumo wa mzunguko wa damu  unaoweza kumuadhiri mama au mtoto. ATHARI ZITOKANAZO NA MAMA MJAMZITO KULALIA MGONGO | CHALI | TUMBO. ∆ Kutokana na damu kushindwa kusafirishwa vizuri inapelekea kumsababishia mama mjamzito kupata matatizo kama, ∆ Kuvimba kwa misuli na inayo ambatana na maumivu (miguu na mikono) ∆ Kushuka au kupanda kwa blood pressure ∆ Ini kuelemewa uzito ∆ Kupunguza mzunguko wa damu ambayo ni hatari kwa uhai wa mtoto ∆ Kusikia kizunguzungu mara kwa mara ∆ Kama kupata kiungulio mara kwa mara nyakati za usiku ∆ Kukoroma ∆ Maumivu ya mgongo ∆ Mama na mtoto ushindwa kupumua vizuri kwa kusosa hewa (oxygen) ∆ Mtoto kukosa virutubi...

ZIFAHAMU DALILI ZA HATARI KWA MAMA MJAMZITO

ZIFAHAMU DALILI ZA HATARI KWA MAMA MJAMZITO Mama mjamzito yuko kwenye hatari ya kupata matatizo mengi yeye na mwanae. Matatizo hayo kujitokeza kwa ishara au dalili tofauti tofauti kulingana na aina ya tatizo alilonalo Mama. DALILI HIZI ZA HATARI KIPINDI CHA UJAUZITO NI . • Kutokwa  na Damu ukeni • Maumivu makali ya Tumbo • Kuhisi kizungu zungu • Maumivu makali ya kichwa • Kutapika sana na kukosa hamu ya kula • Kushindwa kuona • Kupata degedege • Kupata homa kali • Mtoto kuacha kucheza | Kutokucheza siku nzima • Chupa kupasuka bila uchungu kuanza • Kutoa mkojo kidogo Mama mjamzito aonapo Dalili hizi anatakiwa kutoa taarifa haraka na kwenda kituo cha Afya kilicho karibu yake kwa. • Uchunguzi wa kina • Matibabu ya haraka VIPIMO VYA MUHIMU KIPIMA KIPINDI CHA UJAUZITO NI . • Kipimo cha Kaswende • Kipimo cha damu kuangalia wingi wa damu • Kipimo cha mkojo kuangalia wingi wa protini na maambukizi ya njia ya mkojo. • Kipimo cha damu kuangalia gr...

IFAHAMU ARGI PLUS (+) MAANA YAKE | KAZI ZAKE | FAIDA ZAKE | MATUMIZI YAKE

IFAHAMU ARGI PLUS (+) MAANA YAKE | KAZI ZAKE | FAIDA ZAKE | MATUMIZI YAKE FOREVER Argi+ ni bidhaa bora kabisa kutoka katika kampuni yetu ya Forever living products Ina L-arginine amino acid kwa kila kijiko kimoja cha Argi+ Ina Nitric oxide ambayo inasaidia kutanua mishipa ya damu hivyo kuruhusu damu kupita vizuri Ina viondosha sumu vya *POMOGRANATE* ambavyo ni muhimu sana ili kuondoa sumu mwilini Ina *Vitamin* *Complex* ambazo zinasaidia kujenga misuli FAIDA ZA KUTUMIA ARGI+ 1. Ni kirutubisho muhimu sana kutumiwa kila siku kwa ajiili ya kusaidia mifumo yote ya mwili ili kuupa mwili uwezo wa kufanya kazi vizui zaidi. 2. Inasaidia mfumo wa kinga ya mwili, kutokana na nitric oxide ambayo inatumiwa na chembechembe nyeupe za damu kuua bacteria. Hivyo kuupa mwili uwezo zaidi wa kupigana na magonjwa. 3. Inasaidia kurekebisha kiwango cha "blood pressure kiwe sahihi na afya ya mzunguko wa damu ya moyo kiujumla. 4. Inasaidia kutengenezwa kwa mifupa na mwili kiujumla hivyo ...